Facebook
Facebook
You must log in first.
:forum-110833362/smallform/0:
Need a Facebook account?
Help Center
English (US) · বাংলা · हिन्दी · More…
Facebook ©2012

Monday, May 13, 2013

Tigo yazindua Internet ya haraka zaidi Tanzania,4G internet

Meneja Mkuu wa kampuni ya Tigo, Diego Gutierrez( kushoto) akizindua INTANETI YA HARAKA ZAIDI TANZANIA, huduma ya intaneti ya 4G, ambayo ni huduma yenye nguvu zaidi ya vipimo vya hadi 42Mbps itakayowawezesha wateja hao kuperuzi, kupakua na kupakia taarifa mbalimbali kwenye mtandao na kucheza gem kwa haraka zaidi kuliko ilivyokuwa siku za nyuma.Kulia Deon Geyser mfanyakazi kutoka Tigo.

Uzinduzi huo umefanyika kupitia teknologia ya mikutano kwa njia ya mtandao yaani ‘video skype’ iliyounganisha mikoa 4 kwa hotuba maalum iliyokuwa ikitolewa na Ndg. Gutierrez kutoka ofisini kwake makao makuu ya kampuni ya tigo Dar Es Salaam.Mikoa shiriki katika uzindizi huo pamoja na Dar Es Salaam ni Dodoma, Arusha na Morogoro.

Mwanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam akimuuliza swali Meneja Mkuu wa Tigo Tanzania wakati wa uzinduzi huo.

Mwakilishi kutoka kampuni ya Tigo,J OHN SICIMILA (kulia) akimkabidhi William Mganga (katikati) Mshindi wa Samsung S3 phone kupitia ‘raffle droo’ iliyo fanyika katika chuo kikuu cha Dar es Salaam. Kulia ni Lilian Matari msaidizi wa uandaaji wa zoezi hilo.

Waandishi wa habari wa chuo kikuu cha Dar es Salaam wakicheza michezo kwenye Playstation 3 na Waandishi wa habari kutoka Dodoma kupitia kasi mpya ya Intanet ya Tigo yenye ubora nchi nzima.


Mwakilishi kutoka kampuni ya Tigo, JOHN SICIMILA akikabidhi modem mpya za Tigo mmoja wa washindi walioshinda katika michezo ya Playstation 3 kati ya chuo cha DSM na Dodoma.

Waandishi wa habari walipata fursa ya kuzungumza moja kwa moja na Meneja Mkuu wa Tigo Tanzanua Ndg. Guiterrez na maofisa wengine wa Tigo kutoka mikoa hiyo shiriki 4 waliopata fursa ya kutoa maoni yao. 

Kuanzia leo wateja wa tigo wataanza kufurahia huduma ya intaneti ya 4G, ambayo ni huduma yenye nguvu zaidi ya vipimo vya hadi 42Mbps itakayowawezesha wateja hao kuperuzi, kupakua na kupakia taarifa mbalimbali kwenye mtandao na kucheza gem kwa haraka zaidi kuliko ilivyokuwa siku za nyuma.

Meneja mkuu wa tigo Ndg. Diego Gutierrez anasema, “Tunatambua shauku kubwa ya wateja wetu katika kupata huduma iliyobora na ya haraka zaidi ya intaneti, nasi tunajitahidi kadri tuwezavyo, kukidhi kiu yao kwa kuwapatia huduma bora na kwa gharama nafuu zaidi kadri inavyowezekana. Uzinduzi huu ni sehemu tu ya mpango mkakati wetu wa kuboresha mtandao wetu”.

Huduma za kiganjani za intaneti kwa makampuni ya simu ni moja ya huduma muhimu zaidi katika soko la mitandao hiyo na kwa mujibu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), watumiaji wa intaneti Tanzania hadi sasa wanakisiwa kufikia watu milioni 5.

“Kuingiza sokoni kwa vipimo vya 42Mpbs ‘super fast internet speed’ ni ushahidi tosha wa juhudi za tigo za kuongoza makampuni mengine ya simu kwa kuwapatia wateja wetu huduma bora zaidi na za kutosheleza,” alihitimisha Ndg.Gutierrez.

Uzinduzi huo umefanyika kupitia teknologia ya mikutano kwa njia ya mtandao yaani ‘video skype’ iliyounganisha mikoa 4 kwa hotuba maalum iliyokuwa ikitolewa na Ndg. Gutierrez kutoka oficini kwake makao makuu ya kampuni ya tigo Dar Es Salaam. Waandishi wa habari nao walipata fursa ya kuzungumza moja kwa moja na Ndg. Guiterrez na maofisa wengine wa tigo kutoka mikoa hiyo shiriki 4 waliopata fursa ya kutoa maoni yao. Mikoa shiriki katika uzindizi huo ni pamoja na Dar Es Salaam, Dodoma Arusha na Morogoro

Mkutano huo wa waandishi wa habari ulifuatiwa na mashindano ya michezo kwa njia ya mtandao kati ya wanafunzi wa vyuo vikuu viwili nchini Tanzania ambavyo ni Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam na Chuo Kikuu Cha Dodoma ambapo wasomi hao walishindana katika michezo maarufu ya FIFA na ule wa mbio za magari huku washindi wakizawadiwa simu za kisasa za ‘smart phone’ na modemu za spidi kubwa za tigo.

0 comments:

Post a Comment