Facebook
Facebook
You must log in first.
:forum-110833362/smallform/0:
Need a Facebook account?
Help Center
English (US) · বাংলা · हिन्दी · More…
Facebook ©2012

Wednesday, July 31, 2013

MWANAMKE AOZWA KWA NGUVU NA KUBAKWA NA KUNDI LA WANAUME SIKU YA HARUSI...



Mwanamke wa India mwenye miaka 24 amelazimishwa kuolewa na kubakwa na kundi la wanaume kama adhabu ya 'heshima' baada ya kaka yake kutoroka na rafiki yake wa kike, imebainika jana.
Mwanamke huyo - ambaye hakuweza kutajwa kwa usalama wake - aliambiwa anatakiwa kuolewa na mume ambaye ni kaka wa mke wa mchumba mpya wa kaka yake kama 'kisasi' kwa uzinzi wa wawili hao.
Na ndani ya masaa kadhaa za kufunga pingu za maisha na mumewe mpya, akashambuliwa na kubakwa 'bila huruma' na kaka kadhaa wa mchumba wa kaka yake.
Kwa namna ya kushangaza, shambulio hilo ya kutisha lilidaiwa hata kupewa kibali na wazee wa kijiji hicho kilichopo makazi ya vijijini ya Uttar Pradesh, kaskazini mwa India, ambao walidai: "Jicho kwa jicho ni hukumu halisi."
"Ninakubaliana na uamuzi wao sababu ninajua kwamba kungekuwa na umwagaji damu katika kijiji hiki kama ningekataa kuolewa naye," mwanamke huyo aliwaeleza polisi.
"Mashemeji zangu walinibaka bila huruma siku hiyo hiyo niliyofunga ndoa. Ikawa utaratibu wa kawaida.
"Baba mkwe wangu alidai kwamba amekubaliana na ndoa yangu kwa vile alitaka kulipa kisasi (kwa familia yangu) namna hii."
Ajali hiyo mbaya imekuja kujulikana tu pale muathirika alipopata ujasiri wa kufungua madai hayo polisi.
"Machi 26, walifungua kesi dhidi ya kaka yangu na polisi walimkamata yeye na (mke wa mume wangu). Waliachiwa baada ya binti huyo kukiri mbele ya hakimu kwamba aliolewa naye kwa hiari yake," muathirika huyo alidai kwenye madai yake.
Baraza la kijiji au Panchayat, lilidaiwa kumlazimisha mwanamke huyo kuolewa baada ya kaka yake kuwa ametoroka na dada wa mumewe mtarajiwa mnamo Februari 15, mwaka huu.
Panchayat, ambalo liliketi ndai ya siku kumi baada ya kutokomea huko, lilitaka ndoa ya lazima. Mbali na hili, pia liliwataka wazazi wa mwanamke huyo kulipa Rupia 75,000 kama fidia kwa wakwe zake wapya.
Panchayat baadaye lilifafanua hali hiyo iliyojitokeza, likisema 'jicho kwa jicho ni hukumu halisi'.
Watuhumiwa hao wa ubakaji - wanafamilia wanaoshitakiwa -waliripotiwa kuweka bayana kwamba ilikuwa ni ulipizaji wao kisasi kwa kitendo cha utoroshwaji.
Mwanamke huyo kwa namna fulani alifanikiwa kukwepa majaribio yao ya kumkamata Julai 21, mapema asubuhi, na kufungua madai kwa polisi wa Muzaffarnagar mnamo Julai 27.
Mkuu wa polisi, Manzil Saini alisema: "Muathirika huyo amekutana nami. Kesi imefunguliwa chini ya Kifungu 376 ya IPC. Watuhumiwa watakamatwa hivi karibuni."
Kaka mkubwa wa muathirika huyo alidai uamuzi huo uliopelekea tukio hilo ulichukuliwa chini ya usimamizi madhubuti wa Panchayat.
"Polisi walitoa muda kwa watuhumiwa kuondoka kijijini hapo. Mume huyo wa chifu wa panchayat alikuwapo wakati tukio hilo la dada yangu likiamuliwa. Alikuwa msemaji mkubwa na kutaka adhabu kali mno dhidi yetu," alisema.
Mkuu wa panchayat alithibitisha uamuzi wake jana. Alidai aliwataka wafikie suluhisho la amani.
Tukio hilo limekuja wiki mbili baada ya mwanachuo mwenye miaka 20 kubakwa na kundi la wanaume na kisha kuchomwa moto huko Etawah, jimboni Uttar Pradesh, mkoa alikotokea Waziri Mkuu Akhilesh Yadav.
Katika kesi hiyo, kwa namna ya kushitusha, polisi hao si tu kwamba mwanzoni walikataa kufungua kesi lakini pia walionekana kukiuka wajibu wao wa kusimamia sheria na utii.

SOMA HAPA KILICHOMKUTA MADEE ALIPOWASILI NCHINI SOUTH AFRICA

Kwa takribani yapata wikii mbili sasa tokea tuhuma za
madawa ya kulevya kushamili
nchini hususani watanzania wanojishugulisha na maswala hayo....
Karibuni kulizuka tuhuma ambazo za kweli kwa watanzania
kukamatwa na madawa
ya kulevya nchini Afrika ya kusini na hii inaleta mtafaruku ya
ushirikiano wa baina ya
nchi na nchi...
Msanii Madee kutoka Tip Top cinnection jana aliwasili
nchi Afrika ya kusini
na alivyowasili anasema alivyojulikana anatoka Tanzania
aliwekwa pembeni kwa
takribani zaidi ya saa 1 na kusachiwa kuojiwa sana baada ya hapo
kuruhusiwa kuondoka
uwanjani hapo...
Anasema baaada ya kutaja anatokea Tanzania walikuwepo
askari waliovalia sare
walimuamuru kuvua tshirt na kubakia na nguo nyepesi ya
ndani hadi kumkagua
mabegi yake huku abiria aliokuwa amesafiri nao ndege
moja walipita
bila matatizo yoyote...
Sehemu yenyewe ambayo alivuliwa nguo sio kwenye
chumba maalumu
ilikuwa pale pale kwenye mstari,lakini baada ya ukaguzi
walimomba msamaha
na kumruhusu kuendelea na safari yake....!!

Saturday, July 27, 2013

HATIMAYE MBOWE AWASILISHA USHAHIDI WAKE KUHUSU BOMU LA ARUSHA



HATIMAYE Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, jana amewasilisha kwa maandishi ushahidi wake makao makuu ya Jeshi la Polisi mjini Dar es Salaam. Maelezo ya Mbowe ambayo jana yaliwasilishwa, yamekuwa siri nzito, kwani yanatokana na msimamo wa CHADEMA kudai wana ushahidi na tukio la mauaji ya mlipuko wa bomu lililotokea Juni 15, mwaka huu mkoani Arusha.
Wakili wa Mbowe, Peter Kibatala alilithibitishia MTANZANIA mjini Dar es Salaam jana, kuwa aliwasilisha saa 5 asubuhi ambapo alipokelewa na Mkuu wa Idara ya Operesheni za Upelelezi Tanzania (CID), Kamishna Advocate Nyombi.

Baada ya kuwasilisha maelezo hayo, Wakili Kibatala alikataa katakata kuzungumzia kilichomo ndani ya maandishi hayo, kwa madai kuwa ni siri yao na polisi.

“Nathibitisha bila shaka, nimewasilisha majibu kwa niaba ya Mbowe leo (jana), makao makuu ya polisi kama tulivyokubaliana, lakini yaliyoandikwa humo ni siri…siwezi kuzijadili tusubiri kutoka kwao,” alisema Kibatala.

Hatua ya kuwasilisha majibu hayo kimaandishi, ilifikiwa Jumatano wiki hii katika mahojiano baina ya Polisi na Mbowe.

Siku hiyo, Mbowe aligoma kuwasilisha ushahidi wake polisi kama alivyotakiwa kwenye barua aliyoandikiwa na jeshi hilo Julai 17, mwaka huu, kwa kile alichosema hadi Rais Jakaya Kikwete atakapounda tume ya kijaji kuchunguza tukio hilo.

Katika barua hiyo, Mbowe alitakiwa kufika bila kukosa akiwa na ushahidi wa mauaji ya mlipuko wa bomu hilo.

Hata hivyo, Mbowe aliripoti kuitikia wito wa barua hiyo, lakini aliendelea kushikilia msimamo wake wa kutowasilisha ushahidi huo kwa polisi.

Jeshi la Polisi, limekuwa katika mvutano na Mbowe likimtaka kuwasilisha ushahidi kuhusu mlipuko wa bomu hilo, katika Uwanja wa Soweto wakati wa mkutano wa kuhitimisha kampeni za uchaguzi mdogo wa madiwani katika kata nne na kuua watu wanne na kujeruhi wengine 70, katika uwanja huo ushahidi ambao alidai anao.

Endapo Mbowe atakutwa na hatia ya kutokuwa na ushahidi huo, atakumbwa na adhabu ya miaka mitatu jela au faini ya Sh 500,000.

Hii ni kwa mujibu wa Jeshi la Polisi katika barua yake kwa Mbowe, ikunukuu kifungu cha sheria ya kifungu cha 10(2) na (2A) cha sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai nchini, sura ya 20, kama ilivyorekebishwa mwaka 2002.

Wafungwa wa Kitanzania waliokamatwa na madawa ya kulevya Hong Kong wafunguka,Soma Barua walizoandika hapa

 Habari muhimu sana ambazo bado hazijadhibitishwa kuhusiana na biashara ya madawa ya kulevya hapa nchini, lakini naona kama vile haikutiliwa mkazo sana baada ya watu kujikita zaidi kwenye si hasa.nakala ya barua iliyoandikwa Julai 11, 2013 na mfungwa wa Kitanzania kwa niaba ya wafungwa wengine wa Kitanzania waliofungwa huko Hong Kong baada ya kukamatwa na madawa ya kulevya.

Kama barua inavyoonyesha, nakala zimetumwa kwa vyombo vya habari vya Tanzania lakini so far bado sijaisoma hii habari ndani ya vyombo vyetu. Labda bado wanaitafiti na kuthibitisha kama ni ya kweli. Ni vigumu kuthibitisha kama yaliyoandikwa kwenye hiyo barua ni ya kweli lakini nadhani labda ingekuwa vizuri kama vyombo vya habari kujaribu kumwuliza aliyekuwa balozi wetu nchini China, ndugu Phillip Marmo ambaye wafungwa hawa wanadai kwenye barua kuwa alishawahi kuwatembelea huko jela.

Habari kwenye link husika inadai kuwa kuna karibu wafungwa 200 wa Kitanzania waliokamatwa na madawa ya kulevya nchini Hong Kong. Kati ya hao 200, tayari 130 wameshakutwa na hatia na wengine 70 wako mahabusu wakisubiri uchunguzi kukamilika. Inadawaiwa kuwa kati ya Mei and Juni mwaka huu, Watanzania 50 walikamatwa Hong Hong na China kwa kupatikana na madawa ya kulevya. Kwa kawaida wanaokutwa na hatia nchini Hong Kong, wanafungwa kifungo cha miaka 9 kama wakikubali kosa. Wanaokutwa na madawa ya kulevya lakini wakakataa kosa wanafungwa miaka 21 baada ya kudhibitika mahakamani kuwa walikutwa na hayo madawa.

Kama ni kweli, habari iliyopo kwenye hii barua ya Watanzania walioko jela Hong Kong ni mfano halisi wa kinachotokea sehemu nyingine za dunia, kama Afrika ya Kusini na kwingineko. Inategemewa barua hii itasomwa na watu wengi Afrika, hasa Watanzania na itawafanya wengi waache hata kufikiria kuwa punda wa kubebea madawa ya kulevya. Siyo vibaya kama hii barua itaweza kumfanya hata Mtanzania mmoja tuu anayetumika sasa kama punda wa kubebea madawa ya kulevya kuacha kufanya hivyo. Maana kama yaliyoandikwa kwenye hii habari na barua ni ya kweli, basi hali ni mbaya tena sana.

Barua yenyewe hiyo hapo chini. Zipo nakala za aina mbili. Nakala ya kwanza imeandikwa kwa Kiswahili na mfungwa wa Kitanzania kwa niaba ya wafungwa wengine wa Kitanzania huko Hong Kong. Nakala ya pili imetafsiriwa kwa Kiingereza na mfungwa mwingine wa Kitanzania huko huko Hong Kong. Waandishi wa barua wametaja mpaka wahusika wakuu kwenye biashara ya madawa ya kulevya. Kama kweli wanahusika sielewi lakini hawa wanaobeba madawa ya kulevya ndiyo wamewataja


                                     Hapa akawataja baadhi ya wauzaji wa madawa...endelea










                                 Crdts;Mdodosaji

Picha:Kajala masanja akiwa South afrika


Juzi mwigizaji wa bongo movie Kajala aliondokoka nchini kuelekea Afrika ya kusini kwa ajili ya safari binasfi ambayo pamoja na mambo mengine alitembelea shue ya uigizaji ya AFDA (AFDA the South African School of Motion Picture Medium and Live Performance) iliyopo nchini humo.



Magazeti ya leo July 27 2013 haya hapa..


.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
                                      Credits;Millard Ayo

Friday, July 26, 2013

RAY C kurudi tena Stejini mwezi August

Mabibi na mabwana mko tayari kwa ujio mwingine wa Ray- C. Malkia wa kiuno bila mfupa Rehema Chalamila aka Ray-C ametangaza ujio wake rasmi baada ya kuwa chimbo kwa kipindi kirefu toka apate matatizo miezi kadhaa iliyopita.

Ni baada ya siku chache kupita toka Ray-C atamke kuwa anapenda sauti ya ‘dogo lake’ Recho na kuwa atakuja kufanya naye kazi, leo amethibitisha kuwa mwezi Agosti ndio anarudi rasmi kutoka chimboni.

Kupitia akaunti ya Instagram Ray-C aliweka picha ya gazeti moja lililoandika ‘Ray-C kuonekana hadharani mwezi Agosti’, na baada ya followers wake kutaka ufafanuzi ndipo alifunguka kwa kusema “For Sure it’s bout time nw nimewapa muda sana watoto sasa mdada is coming back”.

Ray C aliwauliza marafiki zake wa Instagram kama wapo tayari kwa ‘come back’ yake, wengi wameonekana kutamani muda ufike waweze kumuona tena Ray-C akirudi katika muziki. Hizi ni baadhi ya comments kutoka kwa mashabiki wake.

-The Queen of Bongo Flava is back……yeeeiiii. we cnt wait

-Uuuuuuh i just cant wait

- I real love you mdada, can’t wait to see you again!!

-Nimemic sana naisubiri kwa hamu …nakupenda sana dada angu

-I’m so anxiety about ur comeback, nina kiraruraru heheheheh ebu ukoje to claim back ur throne in the industry

-Heeeheh! Just What I Had On My Mind Yesterday! Like ” @rayc1982 Is Waiting For Ramadhan To Take Back Her Crown” YES Babe!…August Better Hurry!!!

Ray-C aliendelea kujibu maswali ya wengine ambao hawakuamini walichokiona “Very True comin back to take my crown back haleluyah”. Kuna uwezekano baada ya mwezi mtukufu wa Ramadhani Ray-C akatoa wimbo mpya kama ambavyo amethibitisha mwenyewe. Lets wait and see.

KIJIJI CHA MAKAHABA CHAFICHULIWA HUKO KIGAMBONI....MAKAHABA WAPANGISHA NYUMBA NZIMA KWAAJILI YA BIASHARA HIYO..!!

Safari hii imekutana na tukio la aina yake baada ya kumnasa kikongwe mmoja anayedaiwa kumiliki idadi kubwa ya madanguro katika uwanja wake na kuwapangisha makahaba katika eneo maarufu kwa jina la Kijiji cha Makahaba. 




Awali kachero wa OFM alipokea ujumbe mfupi ulioelezea ufuska unaofanywa na mabinti ambao hupewa eneo na kujenga vibanda kisha kujiuza kwa bei chee katika kijiji hicho maeneo ya Kigamboni jijini Dar.



Mzee Matutu ambaye ni mmiliki wa eneo linalofanyiwa ufuska.
Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kwamba, eneo hilo linalofanyiwa ufuska huo linamilikiwa na kikongwe aliyejitambulisha kwa jina la mzee Matutu akidaiwa kuendesha maisha kwa biashara hiyo ya madanguro.



Baada ya kujiridhisha na uchunguzi kuwa ni kweli jambo hilo linafanyika eneo hilo, OFM ililivamia ikiwa na mjumbe wa mtaa huo aliyefahamika kwa jina la Abbas na kujionea madanguro yaliyojengwa kwa mstari ambapo milango yake iliachwa wazi huku ndani wakionekana mabinti wakiwa wamejilaza kihasarahasara wakiwatega wateja wanaopita katika mtaa huo.
Madanguro hayo ambayo kwa hesabu ni takriban kumi na nane, yamejengwa kwa aina yake ambapo mengi kati ya hayo yana ukubwa wa kutosha kuingia kitanda kidogo pekee.




Baada ya kujionea hayo, kikosi kazi sambamba na mjumbe huyo kilimtafuta mzee Matutu na kufanikiwa kuzungumza naye kuhusu madanguro hayo na namna anavyoyaendesha ambapo alikiri kuwa yeye ni mmiliki wa eneo hilo na huwa anapokea shilingi 30,000 kwa mwezi kwa kila mwanamke na fedha hiyo ndiyo inayomsaidia kuendesha maisha.
Sina kazi nyingine ya kuniingizia kipato zaidi ya hii ya wasichana licha ya kwamba sijawaruhusu wafanye biashara hiyo. Fedha hiyo ndiyo inanisaidia kwa mahitaji yang
ualisema kwa tabu mzee Matutu huku akimtaja msimamizi wa madanguro hayo kuwa ni mpwa wake.
Kwa upande wake mjumbe wa mtaa huo, Kassim alisema kuwa serikali ya mtaa imejitahidi kwa kadiri ilivyoweza kuwaondoa mabinti hao lakini wamekuwa wakirudi kila mara.
Alipoulizwa hatua waliyoichukua kwa mmiliki wa madanguro hayo ambaye ni mzee Matutu, kiongozi huyo alibakia kusikitika asijue hatua gani ya kumchukulia mzee huyo ambaye hata wakimpeleka kwenye vyombo vya sheria anahisi itakuwa ni uonevu kwa kuwa hana msaada mwingine wa kifedha zaidi ya fedha kutoka kwa mabinti hao.


         Credits;SwahiliTZ

"NILIJUA TU KWAMBA WANAFIKI WATAFURAHIA MATESO YANGU" ....AGNESS MASONGANGE

VIDEO Queen ambaye hivi karibuni alidaiwa kukamatwa na madawa yanayosadikiwa ni ya kulevya ‘unga’ nchini Afrika Kusini ‘Sauzi’, Agness Gerald ‘Masogange’ amefunguka kuwa alijua watu wengi watafurahia kilichompata kwa kumuongelea kila wakati.

Akizungumza na mwanahabari wetu kwa njia ya simu akiwa Sauzi, Masongange ‘alishauti’ kuwa watu wengi wanamuongelea vibaya bila kujua nini kilichompata  hivyo anaamini hata marafiki zake wa karibu wamefurahia tatizo alilopata.


“Najua kabisa kuna watu wengi wamefurahia tatizo nililopata lakini watambue kuwa kila mtu anaweza kupata tatizo hivyo wapunguze kuongea sana bila kujua ni kitu gani kilichotokea juu yangu,” alisema Masogange ambaye atapanda kizimbani kwa mara ya pili mwezi ujao.

Monday, July 22, 2013

Wafumaniwa wakifanya mapenzi na kuku

Nchini Kenya katika kijiji cha Kigwandi, wilayani ya Tetu, mwanaume mmoja anashilikiliwa katika kituo cha polisi baada ya kufumaniwa akifanya mapenzi na kuku.

Mwanamume huyo mwenye umri wa zaidi ya miaka 50 alikamatwa akifanya kitendo hicho na kuku juzi jioni na mwanae mwenye umri wa miaka 10 aliyeamua kumwita kaka yake na ndipo ikasaidia kukamatwa kwa mtu huyo.

Kaimu afisa mkuu wa polisi katika eneo hilo, Joseph Mwika alisema mtoto wa jamaa huyo alimuarifu ka’kake mkubwa baada ya kumfumania babake akifanya kitendo hicho na wawili hao walimripoti baba yao kwa chifu wa eneo hilo ambaye alimkamata na kumpeleka katika kituo cha polisi.
source:Standard Digital,kenya

Sunday, July 21, 2013

Eti Boyfriend wangu anajua mi ni bikra...Mhhh angejua!

I am a 22-year-old university student. I came to university with my v*rg*nity intact.

After being here for a few months, I am no longer a v*rg*n and I have had s*x with three different guys, none of them I can call my boyfriend. I have a boyfriend. He is five years older than I am. We were both Christians. We kissed but never had s*x. I can no longer consider myself a Christian. Whenever he calls me, I don't know what to talk to him about because I feel so guilty. I told him he should forget me because I have changed, but I didn't tell how I have.

My roommate got me into drinking and having s*x with guys. One weekend my roommate had s*x with two different guys. We talked about it. Sometimes she goes to the guys' room and have s*x with them. I love her because she is good to me. I suffer from pr*m*nstrual pain and she helps me during my time of the month. Sometimes I think she has made me a very bad girl.

My boyfriend still thinks I am a v*rg*n. Should I still tell him I am not and he should take his mind off me?

HIZI NDO TIMU TAJIRI ZAIDI DUNIANI KWA MUJIBU WA FORBES MAGAZINE


1 Real Madrid
Value: $3.3 billion
Owner: Club members

2 Manchester United
Value: $3.165 billion
Owner: Glazer family

#3 Barcelona
Value: $2.6 billion
Owner: Club members

#4 New York Yankees
Value: $2.3 billion
Owner: Steinbrenner Family

#5 Dallas Cowboys
Value: $2.1 billion
Owner: Jerry Jones


#6 New England Patriots
Value: $1.635 billion
Owner: Robert Kraft

#7 Los Angeles Dodgers
Value: $1.615 billion
Owner: Guggenheim Baseball

#8 Washington Redskins
Value: $1.6 billion
Owner: Daniel Snyder

#9 New York Giants
Value: $1.468 billion
Owners: John Mara, Steven Tisch

#10 Arsenal
Value: $1.326 billion
Owner: Stan Kroenke