Facebook
Facebook
You must log in first.
:forum-110833362/smallform/0:
Need a Facebook account?
Help Center
English (US) · বাংলা · हिन्दी · More…
Facebook ©2012

Saturday, May 18, 2013

NISHA AMKIMBIZA WEMA KWA KUMILIKI NYUMBA YA KIFAHARI, HII NDO NYUMBA YA NISHA YENYE THAMANI YA MILIONI 95. ICHEKI HAPA


Stori:Gladness Mallya
Unakumbuka zile habari za Wema Isaac Sepetu kununuliwa jumba la kifahari na bilionea mmoja Kijitonyama, Dar? Sasa zimegeukia kwa staa wa sinema za Kibongo, Salma Jabu ‘Nisha’ ambaye naye kuna madai mazito ya kuhongwa nyumba.

Ilikuwa mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo gazeti hili lilipokea ujumbe mfupi wa simu ya mkononi ‘sms’ kutoka kwa chanzo chake.
HABARI ILIVYOANZA
Chanzo: Hivi ninyi mna habari?
Risasi Jumamosi: Nyingi tu lakini kama una ya kwako itatufaa sana.
Chanzo: Kwa taarifa yenu Nisha kanunuliwa bonge la mjengo hapa Kijitonyama karibu kabisa na Kituo cha Polisi cha Kijitonyama ‘Mabatini’.
Risasi Jumamosi: Nani kamnunulia?
Chanzo: Nasikia ni bilionea mmoja mwenye fedha zake hapa Dar es Salaam, kainunua kisha kamhonga Nisha kwa sababu ni mpenzi wake.
Risasi Jumamosi: Tunashukuru kwa taarifa, kaa mkao wa kula itaruka hewani mara moja baada ya upelelezi wetu.
RISASI LATUA KIJITONYAMA
Baada ya kuzinyaka habari hizo, gazeti hili lilisaga soli hadi maeneo hayo na kuanza kugonga geti moja baada ya lingine hadi lilipofanikiwa kuinasa nyumba hiyo huku Nisha akiwa ndani kapumzika.
Msichana aliyejitambulisha kuwa ni dada wa kazi au hausigeli kwa lugha laini ndiye aliyetoboa siri kuwa ni kweli staa huyo yupo ndani na amehamia mahali hapo muda si mrefu.
RISASI LAINGIA MJENGONI
Risasi Jumamosi liliomba kukaribishwa ndani ili kupata ‘ditelzi’ na ndipo Nisha akaamka na kuamua kuacha paparazi wetu apige picha japo awali alitia ngumu akidai hayuko tayari kuianika nyumba hiyo.
Ndani ya nyumba hiyo yenye vyumba vitano, sebule, jiko, choo na mabafu mawili, anayeishi Nisha na dada wake wa kazi, kuna samani nyingi za bei mbaya, mazagazaga kibao, mazulia na marumaru huku kila kona kukiwa na Tv ya flat screen hadi chooni (angalia picha Uk.1).
NISHA ABANWA KUHUSU UMILIKI
Nisha anayemiliki kampuni ya kuzalisha muvi za Kibongo ya Nisha’s Film Production alipotakiwa kueleza kama kanunua, kanunuliwa au kapangisha nyumba hiyo, alikuwa na haya ya kusema:
“Ni juhudi zangu binafsi jamani, kujituma sana kwenye kazi yangu ya filamu. Kuhusu kununua au kupangisha naomba nikimaliza ‘process’ f’lanif’lani ndipo nitaweka wazi, kwa sasa bado ni mapema mno.”
Risasi Jumamosi: Kuna madai kuwa umehongwa hii nyumba na bilionea mmoja wa hapa Dar, je, ni kweli?
Nisha: Hakuna kitu kama hicho jamani, hayo ni maneno ya watu wasiojituma kufanya kazi kwa bidii. Haya ni matunda ya kufanya kazi sana.
Risasi Jumamosi: Nyumba hii ina samani mpya zote za thamani kubwa sana, je, zimegharimu fedha kiasi gani?
Nisha: Vitu vyote vya ndani hadi nikahamia vimegharimu karibu Sh. milioni 95. Ni fedha zilizotokana na mauzo ya filamu zangu nne nilizotengeneza mwenyewe mwaka jana.
Risasi Jumamosi: Kuna madai kuwa umejiunga Freemason ndiyo maana ndani ya kipindi kifupi mambo yako safi, je, ni kweli?
Nisha: Nimesikia hizo tetesi za Freemason ‘but’ naamini mti wenye matunda ndiyo hupigwa mawe. Mimi namwachia Mungu, namuomba kila siku anipe baraka zake, namshukuru na nazidi kumuomba nifanikiwe.TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

0 comments:

Post a Comment