Stori:Gladnees Mallya
BABA wa marehemu Steven Kanumba, mzee
Charles Kanumba amefunguka kuwa haoni ulazima wa kuliona kaburi la
mwanaye na kuhusu kufanya maombi mwaka mmoja baada ya kifo, alifanya
akiwa huko nyumbani kwake Shinyanga.
Akizungumza na Ijumaa kwa njia ya
simu hivi karibuni, mzee Charles alisema mtu anapofariki kikubwa ni
kuombewa na hilo la kwenda kulitazama kaburi lake haliwezi kuwa na
faida.
“Mimi nilifanya sala ya kumuombea
Kanumba pamoja na mtoto wa dada yake ambaye walikufa kwa kufuatana
kwenye Kanisa la AIC Shinyanga,” alisema mzee huyo na kuongeza;
“Mtu akishakufa kinachobaki ni
kumuombea huko aliko na kaa ukijua kwamba huku ndiyo kwenye chimbuko la
marehemu hivyo nisingeweza kwenda kufanyia maombi kwenye mji mwingine.”
Chanzo:www.globalpublishers.info
0 comments:
Post a Comment