Wachezaji wawili wa Ivory Coast
wametimuliwa kwenye kikosi kinachojiandaa
na mchezo kuwania kufuzu michuano ya
kombe la dunia mwaka 2014 dhidi ya
Tanzania unaotarajiwa kupigwa uwanja wa
Taifa siku ya Jumapili.
Mchezaji wa zamani wa Monaco Jean-Jacques
Gosso Gosso, 30, ambaye kwa sasa
anakipiga kwenye ligi ya Uturuki akiichezea
Mersin na kinda la miaka 20 Abdul Razack wa
Manchester City, ambaye kwa sasa yupo kwa
mkopo Charlton Athletic, walipigana siku ya
jumatano wakati timu yao ikiwa kwenye
maandalizi ya mwisho kabla ya kuelekea
Tanzania usiku wa leo.
FA ya Cote D’Ivoire imesema kwamba adhabu
nyingine zinaweza kufuatiwa kutegemea na
kamati ya nidhamu itakavyoamua.
source -shafiidauda
0 comments:
Post a Comment