Facebook
Facebook
You must log in first.
:forum-110833362/smallform/0:
Need a Facebook account?
Help Center
English (US) · বাংলা · हिन्दी · More…
Facebook ©2012

Thursday, November 21, 2013

Sababu za Adan Rage kusimamishwa Adan Rage wazijua?Zisome hapa..Uongozi umezifafanua zaidi.

Jana uongozi wa klabu ya Simba ulitangaza kumsimamisha mwenyekiti wake Ismail Aden Rage.
Maamuzi hayo yalitokana na kikao cha kamati ya utendaji kilichofanyika hapo juzi,
Hizi ni Miongoni mwa sababu zilizotolewa kwenye mkutano wa waandishi wa habari zilizopelekea kusimamishwa kwa Mheshimiwa Rage.
Mkataba na AZAM  TV
Rage alisaini mkataba na Azam TV kwa ajili ya kipindi ya cha Simba TV bila kuishirikisha kamati ya utendaji.
Wakati Rage anasaini mkataba na Azam TV tayari klabu ya Simba ilikuwa kwenye mazungumzo ya mwisho mwisho kuingia mkataba na kampuni ya ZUKU kwa ajili kipindi cha Simba TV uliokuwa na thamani ya dola za kimarekani 300,000 kwa mwaka.
Kampuni ya ZUKU ilipokuwa kwenye majadiliano na viongozi wa vilabu vya Simba na Yanga jijini Nairobi, kwenye mkutano huo Simba iliwakilishwa na Mjumbe wa kamati ya utendaji Joseph Itang’are maarufu kama mzee Kinesi pamoja na mwanachama Evans Aveva wakati Yanga iliwakilishwa na Makamu mwenyekiti Clement Sanga na Francis Kifukwe,viongozi hao Simba Ghafla walisikia Rage kasaini mkataba na Azam TV kwa ajili ya Simba TV.
Sakata la uhamisho wa Emmaanuel Okwi.
Mheshimiwa Rage ndiye aliyesimamia uhamisho wa mchezaji Okwi on CREDIT bila kuishirikisha kamati ya utendaji,matokeo yake klabu hiyo mpaka leo imeshindwa kupata pesa ya uhamisho wa mchezaji huyo.
.
Kutoitisha vikao vya kamati ya utendaji.
Sababu nyingine iliyoelezwa ni kitendo chake cha kushindwa kuitisha vikao vya kamati ya utendaji, Kuendesha klabu na kufanya maamuzi binafsi bila ya kushirikisha kamati hiyo ya utendaji ambayo ilichaguliwa na wanachama
Strategic plan ( Mpango mkakati )
Hivi karibuni klabu ya Simba ilizindua mchakato wa kutengeneza mpango mkakati (Strategic Plan) lakini cha kushangaza mwenyekiti amekuwa hataki kuona mpango huo ukifanikiwa.
Mkutano mkuu wa katiba

Kushindwa kuitisha mkutano wa marekebisho ya katiba,kuchukua maamuzi binafsi ya kuhairisha mkutano maalumu wa katiba uliotakiwa kufanyika Novemba, mwaka huu.

0 comments:

Post a Comment