
Timu ya kuchunguza tukio la kutekwa na
kuumizwa kwa Mwenyekiti wa Jukwaa
la Wahariri Tanzania (TEF), Absalom
Kibanda (pichani), imebaini kuwa kazi
yake ya uandishi wa habari na siasa
vimechangia kuvamiwa kwake na kuna
kutupiana mpira kati ya vyombo vya
dola na vyama vya siasa. Aidha,
uchunguzi wa timu hiyo umebainisha
kuwa baadhi ya watu waliohojiwa
walidai kuwa utekaji wa Kibanda
ulifanywa na vyombo vya dola ukiwa
sehemu ya mpango mkakati wa vyombo
hivyo...